Zaburi 67

1 Mungu aturehemu na kutubariki, na kutuangazia nuru za uso wake,

2 ili njia zako zijulikane duniani, wokovu wako katikati ya mataifa yote.

3 Ee Mungu, mataifa na wakusifu, mataifa yote na wakusifu.

4 Mataifa yote wafurahi na kuimba kwa shangwe, kwa kuwa unatawala watu kwa haki na kuongoza mataifa ya dunia.

5 Ee Mungu, mataifa na wakusifu, mataifa yote na wakusifu.

6 Ndipo nchi itatoa mazao yake, naye Mungu, Mungu wetu, atatubariki.

7 Mungu atatubariki na miisho yote ya dunia itamcha yeye.