Zaburi 124
1 Kama Mwenyezi Mungu hangekuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:
2 kama Mwenyezi Mungu hangekuwa upande wetu, watu walipotushambulia,
3 hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangetumeza tukiwa hai,
4 mafuriko yangegharikisha, maji mengi yangetufunika,
5 maji yaendayo kasi yangetuchukua.
6 Ahimidiwe Mwenyezi Mungu, ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.
7 Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tumeokoka.
8 Msaada wetu ni katika jina la Mwenyezi Mungu, Muumba wa mbingu na dunia.