Zaburi 3
1 Ee Mwenyezi Mungu, tazama adui zangu walivyo wengi! Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
2 Wengi wanasema juu yangu, “Mungu hatamwokoa.”
3 Lakini wewe, Ee Mwenyezi Mungu, ni ngao yangu pande zote; umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
4 Ninamlilia Mwenyezi Mungu kwa sauti kuu, naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.
5 Ninajilaza na kupata usingizi; naamka tena, kwa maana Mwenyezi Mungu hunitegemeza.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui, wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
7 Ee Mwenyezi Mungu, amka! Niokoe, Ee Mungu wangu! Wapige adui zangu wote kwenye taya, vunja meno ya waovu.
8 Kwa maana wokovu watoka kwa Mwenyezi Mungu. Baraka yako na iwe juu ya watu wako.