Zaburi 14
1 Mpumbavu anasema moyoni mwake, “Hakuna Mungu.” Wamepotoka, matendo yao ni maovu kabisa; hakuna hata mmoja atendaye mema.
2 Mwenyezi Mungu anawachungulia wanadamu kutoka mbinguni aone kama kuna mwenye hekima, yeyote anayemtafuta Mungu.
3 Wote wamepotoka, wote wameoza pamoja; hakuna atendaye mema, naam, hakuna hata mmoja!
4 Je, watendao maovu kamwe hawatajifunza: wale ambao huwala watu wangu kama watu walavyo mkate, hao ambao hawamwiti Mwenyezi Mungu?
5 Wako hapo, wameingiwa na hofu kuu, maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
6 Ninyi watenda maovu mnakwamisha mipango ya maskini, bali Mwenyezi Mungu ndiye kimbilio lao.
7 Laiti wokovu wa Israeli ungekuja kutoka Sayuni! Mwenyezi Mungu anaporejesha wafungwa wa watu wake, Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!