Zaburi 114

1 Israeli alipotoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa watu wa lugha ngeni,

2 Yuda alifanywa makao matakatifu ya Mungu, Israeli akawa milki yake.

3 Bahari ilitazama ikakimbia, Yordani ulirudi nyuma,

4 milima ilirukaruka kama kondoo dume, vilima kama wana-kondoo.

5 Ee bahari, ni nini kilichokufanya ukakimbia, nawe, ee Yordani, ukarudi nyuma,

6 enyi milima mkarukaruka kama kondoo dume, enyi vilima, kama wana-kondoo?

7 Ee dunia, tetemeka mbele za Bwana, mbele za Mungu wa Yakobo,

8 aliyegeuza mwamba kuwa dimbwi la maji, mwamba mgumu kuwa chemchemi za maji.