Zaburi 13
1 Hadi lini, Ee Mwenyezi Mungu? Je, utanisahau milele? Utanificha uso wako hadi lini?
2 Nitapambana na mawazo yangu hadi lini, na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu? Adui zangu watanishinda hadi lini?
3 Nitazame, unijibu, Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wangu. Yatie nuru macho yangu, ama sivyo nitalala usingizi wa mauti.
4 Adui yangu atasema, “Nimemshinda,” nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.
5 Lakini ninategemea upendo wako usiokoma; moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
6 Nitamwimbia Mwenyezi Mungu, kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.