Zaburi 6
1 Ee Mwenyezi Mungu, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Unirehemu Mwenyezi Mungu, kwa maana nimedhoofika; Ee Mwenyezi Mungu, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
3 Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Hadi lini, Ee Mwenyezi Mungu, hadi lini?
4 Geuka, Ee Mwenyezi Mungu, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa Kuzimu?
6 Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha natiririsha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha kiti changu kwa machozi yangu.
7 Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Mwenyezi Mungu amesikia kulia kwangu.
9 Mwenyezi Mungu amesikia kilio changu kwa huruma, Mwenyezi Mungu amekubali sala yangu.
10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma na waaibishwe kwa ghafula.