Zaburi 87
1 Ameuweka msingi wake katika mlima mtakatifu;
2 Mwenyezi Mungu anayapenda malango ya Sayuni kuliko makao yote ya Yakobo.
3 Mambo matukufu yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:
4 “Nitaweka kumbukumbu ya Rahabu na Babeli miongoni mwa wale wanaonikubali mimi: Ufilisti pia na Tiro, pamoja na Kushi, nami nitasema, ‘Huyu alizaliwa Sayuni.’ ”
5 Kuhusu Sayuni itasemwa hivi, “Huyu na yule walizaliwa humo, naye Aliye Juu Sana mwenyewe atamwimarisha.”
6 Mwenyezi Mungu ataandika katika orodha ya mataifa: “Huyu alizaliwa Sayuni.”
7 Watakapokuwa wanapiga vinanda wataimba, “Chemchemi zangu zote ziko kwako.”