Zaburi 20

1 Mwenyezi Mungu na akujibu unapokuwa katika dhiki, jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.

2 Na akutumie msaada kutoka patakatifu na akupatie msaada kutoka Sayuni.

3 Na azikumbuke dhabihu zako zote, na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.

4 Na akujalie haja ya moyo wako, na aifanikishe mipango yako yote.

5 Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda, tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu. Mwenyezi Mungu na akupe haja zako zote.

6 Sasa nafahamu kuwa Mwenyezi Mungu humwokoa mpakwa mafuta wake, humjibu kutoka mbingu yake takatifu kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.

7 Wengine wanatumaini magari ya vita, na wengine farasi, bali sisi tutalitumainia jina la Mwenyezi Mungu, Mungu wetu.

8 Wao wameshushwa chini na kuanguka, bali sisi tunainuka na kusimama imara.

9 Ee Mwenyezi Mungu, mwokoe mfalme! Tujibu tunapokuita!