Zaburi 128

1 Heri wale wote wamchao Mwenyezi Mungu, wanaoenda katika njia zake.

2 Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.

4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Mwenyezi Mungu.

5 Mwenyezi Mungu na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,

6 nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.